islamkingdomface islamkingdomtwitte islamkingdominstagram islamkingdompinterest islamkingdomtumblr islamkingdomreddit islamkingdomvk


SWALA YA KUOMBA MVUA


9220
wasifu
Ukame ni alama ya watu kuwa mbali na Utiifu kwa Mwenyezi Mungu (SW) na ishara wazi yakukithiri maasi. Kumuasi Mwenyezi Mungu (SW) kunaleta shari na kunafuta Baraka. Na miongoni mwa rehema zake kwa waja wake na kule kuwawekea Swala ya kuomba mvua, wakapata kurudi kwa Mola wao na kutaka msamaha kwake awaondolee shida waliyonayo, ili mvua iwateremkie ikiwa ni rehema kutoka Kwake kwa waja wake.
Khutba ya

Kila ugonjwa una tiba yake, ardhi ikiwa kavu na kupatikana ukame. Uislamu unamaanisha kuswali swalatul Istiskai nayo ni Swala ya kumuomba Mwenyezi Mungu kuteremsha mvua. Leo Swala hii imesahulika kabisa katika Umma wa kislamu. Waislamu wakipata matatizo ya uhaba wa Mvua, moja kwa moja wanaelekea kuomba majini na mashetani. Mafundisho ya Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) yako wazi kabisa kuwaelekeza Waislamu katika njia ya Allah (Subhaanahu wa Taala) wakati wowote na hali yoyote sawa wakati wa raha au shida. Kumtii Mwenyezi Mungu ndio mambo yote. Amesema Mwenyzi Mungu (Subhaanahu wa Taala) :

قال تعالى) : وَلَوْ أَنَّهُمْ أَقَامُوا التَّوْرَاةَ وَالْإِنْجِيلَ وَمَا أُنْزِلَ إِلَيْهِمْ مِنْ رَبِّهِمْ لَأَكَلُوا مِنْ فَوْقِهِمْ وَمِنْ تَحْتِ أَرْجُلِهِمْ مِنْهُمْ أُمَّةٌ مُقْتَصِدَةٌ وَكَثِيرٌ مِنْهُمْ سَاءَ مَا يَعْمَلُونَ) [المائدة: 66] {{Na kama wangalisimamisha Taurati na Injili na yale yaliyoteremshwa kwao kutoka kwa Mola wao, kwa yakini wangalikula vya juu yao na vya chini ya miguu yao. Lakini wako watu miongoni mwao washikao njia nzuri. Lakini wengi wao wanayoyafanya ni mabaya kabisa}}.

Na Amesema Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala):

قال تعالى : (وَلَوْ أَنَّهُمْ أَقَامُوا التَّوْرَاةَ وَالْإِنْجِيلَ وَمَا أُنْزِلَ إِلَيْهِمْ مِنْ رَبِّهِمْ لَأَكَلُوا مِنْ فَوْقِهِمْ وَمِنْ تَحْتِ أَرْجُلِهِمْ مِنْهُمْ أُمَّةٌ مُقْتَصِدَةٌ وَكَثِيرٌ مِنْهُمْ سَاءَ مَا يَعْمَلُونَ ) [المائدة: 66]

{{Nikawaambia; Ombeni msamaha kwa Mola wenu. Hakika Yeye ni Mwingi wa msamaha. Atakuleteni mawingu yanyeshayo mvua nyingi}}.

Na akasema tena Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala):

قال تعالى) : وَلَوْ أَنَّ أَهْلَ الْقُرَى آَمَنُوا وَاتَّقَوْا لَفَتَحْنَا عَلَيْهِمْ بَرَكَاتٍ مِنَ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ وَلَكِنْ كَذَّبُوا فَأَخَذْنَاهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ )[الأعراف: 96] {{Na lau kama watu wa miji wangaliamini na kuogopa, kwa yakini tungaliwafungulia baraka za mbingu na ardhi. Lakini walikadhibisha; tukawapatiliza kwa sababu ya yale waliyokuwa wakiyachuma}}.

Kumuasi Mwenyezi Mungu ndio sababu ya kuleta shari na kuondoka kwa baraka.

Amesema Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala):

 

قال تعالى) : وَالَّذِينَ إِذَا فَعَلُوا فَاحِشَةً أَوْ ظَلَمُوا أَنْفُسَهُمْ ذَكَرُوا اللَّهَ فَاسْتَغْفَرُوا لِذُنُوبِهِمْ وَمَنْ يَغْفِرُ الذُّنُوبَ إِلَّا اللَّهُ وَلَمْ يُصِرُّوا عَلَى مَا فَعَلُوا وَهُمْ يَعْلَمُونَ) [آل عمران: 135] {{Na ambao wanapofanya uchafu au kudhulumu nafsi zao, hukumbuka Mwenyezi Mungu na kuomba msamaha kwa dhambi zao. Na nani anayesamehe dhambi isipokuwa Mwenyezi Mungu}}.

Ametaja Ibn Qayyim baadhi ya maafa yanayoletwa na maasi; huleta udhalifu, huharibu akili, huwaondosha haya, hudhoofisha moyo, huondosha neema, hutia maradhi moyo, huleta nuksi, hupotosha ya moyo, hufanya moyo kuwa mdogo, huondosha karama, pia Baraka, na kulaumiwa, kutishika, huondosha hima ya kumcha Mwenyezi Mungu.

Ukame ni alama ya kuwa watu mbali na twaa ya Mwenyezi Mungu, na ishara ya kuzidi maasi. Hali ya anga inabadilika kutokana na maasi.

Amesema Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala):

قال تعالى): ظَهَرَ الْفَسَادُ فِي الْبَرِّ وَالْبَحْرِ بِمَا كَسَبَتْ أَيْدِي النَّاسِ لِيُذِيقَهُمْ بَعْضَ الَّذِي عَمِلُوا لَعَلَّهُمْ يَرْجِعُونَ ) [الروم: 41]

{{Uharibifu umedhihiri barani na baharini kwa sababu ya yale iliyoyafanya mikono ya watu, ili Awaonjeshe adhabu ya baadhi ya mambo waliyofanya, huenda wakarudi wakatubia kwa Mwenyezi Mungu}}.

Na anasema Anas bin Malik: Upepo ukiwa mkali hujulikana hilo kwa uso wa Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam). Amepokea Abu Huraira hadithi: kutoka kwa Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) akisema: [Hakisimami Qiyama mpaka iondoke ilimu, na kuzidi Zilzaal, na zahama kuwa karibu, na kudhihiri fitna, na kuzidi mauaji, mpaka itakua kwenu mali nyingi]. Ufupisho ni kujirudi nafsi, na kuomba msamaha kwa Allah pamoja na kufuata sheria za Allah (Subhaanahu wa Taala).

Amesema Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala):

قال تعالى) : يُنَبَّأُ الْإِنْسَانُ يَوْمَئِذٍ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ13 بَلِ الْإِنْسَانُ عَلَى نَفْسِهِ بَصِيرَةٌ 14وَلَوْ أَلْقَى مَعَاذِيرَهُ 15)[القيامة13: 15]

{{Siku hiyo ataambiwa mwanadamu aliyotanguliza na aliyoyaakhirisha. Bali mtu ni shahidi juu ya nafasi yake}}.

Na neno lake Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) akisema: [Tunajilinda na Mwenyezi Mungu kutokana na uovu wa nafsi zetu, na uovu wa matendo yetu]. Imepekewa kwa Masahaba wakisema: Alitusalisha Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) swala ya usubuhi Hudeibiyah kukiwa na mawingu usiku, baada ya hapo akatukabili na kusema: Je mnajua alivyosema Mwenyezi Mungu? Wakajibu maswahaba: Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanajua. Akasema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam): [ Baadhi ya waja wangu wamekua waumini ni wale waliosema tumeteremshiwa mvua kutokana na fadhila zake Mwenyezi Mungu, na makafiri tumeteremshiwa mvua kutokana na nyota fulani].

Khutba ya pili
>Namna ya kuswali Swala ya Istiskai (Swala ya Mvua)

Ametoka ‘Abdillah ibn Yazid pamoja na Burai Bin ‘Azib na Zeid Bin Arkam kuswali ya Swala ya istiskai, akasimama na kumuomba Mwenyezi Mungu msamaha, kisha wakaswali rakaa mbili, kudhihirisha kisomo, bila adhani wala ikama. Na kama alivyopokea ‘Abdillah bin Zaid kwamba Mtme (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) ameswali swala ya Istiskai kuelekea kibla, na kugeuza kishali chake na kuswali rakaa mbili. Amepokea Anas Bin Malik kuwa Mtume hainui mkono wake anapo omba isipokuwa katika swala ya istiskai, na alikuwa akiinua mkono wake mpaka ikionekana weupe wa makwapa yake.

Na ni sunna kuwalingania Waislamu wote kumcha Mwenyezi Mungu na kutaka radhi zake Mwenyezi Mungu kwa kutoa sadaka na kuunga kizazi. Amepokea Anas Bin Malik akisema: nimemsikia Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) akisema: [ Amesema Mwenyezi Mungu ewe mwanaadamu unaponiomba na ukataraji kutoka kwangu nitakusamehe kwa yale uliyo nayo bila kujali, ewe mwanaadamu madhambi yako yakafika mbinguni kisha ukaniomba msamaha nitakusamehe. Ukifanya madhambi kiasi cha ‘arshi na hukunishirikisha Mwenyezi Mungu nitakusamehe madhambi hao]. Walipopatwa Makureish na ukame na kula mfu na mifupa. Abu Sufyan alikwenda kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu na kumuambia: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu umetuamrisha kuunga kizazi. Na waja wako wanaangamia, tuombee Mungu. Mtume wa Mwenyezi Mungu akaomba, ikateremka Mvua mpaka wakaogopa watu.

Amesema Hassan Basri: ‘Zidisheni kutaka msamaha kwa Mwenyezi Mungu nyumbani kwenu, kwenye meza zenu, njiani, sokoni, makao yenu, na popote mlipo, kwani hamjui wakati gani utashuka msamaha wa Allah.

Mwisho

Ndugu katika Imani, Sababu kubwa ya kukosekana mvua ni kudhihiri machafu baharini na nchi kavu. Ili tuweze kupata rehma ya Mwenyezi Mungu na kuteremshiwa mvua kutoka mbiguni ni wajibu juu ya kila Muislamu kurudi kwa Allah kwa kuomba msamaha na kuendelea kufanya mambo ya kheri na kujiepusha na mambo mabaya.

Tunamuomba Mwenyezi Mungu Atuteremshie mvua na rehma na Baraka. Naelekeza wito wangu kwa watu wote kumuomba Mwenyezi Mungu Atubariki. Namuomba Mwenyezi Mungu kuteremsha mvua na kuwarehemu waja wake na miji yake.





Vitambulisho: