islamkingdomface islamkingdomtwitte islamkingdominstagram islamkingdompinterest islamkingdomtumblr islamkingdomreddit islamkingdomvk


UMUHIMU WA SWALA KATIKA UISLAMU


13449
wasifu
swala ni nguzo ya pili katika uislamu baada ya shahada,na ni amali ya kwanza atakayo ulizwa siku ya kiyama swala ikiwa mzuri basi amali zake zote nyingine zitakuwa mzuri na swala ikiwa ni mbaya basi amali zake nyingine zitakuwa mbaya,na swala ni ndio inamtafautisha muislamu na asiekuwa muislamu ,na mwenye kuisimamisha swala huwa amesimamisha dini na mwenye kuacha swala huwa ameivunja dini
Khutba ya

Dini ya kiislamu ambayo Mwenyezi Mungu ameitukuza na kuridhia nayo, na ameweka malipo makubwa kwa vile vinavyotamani nafsi na uislamu umejengwa na misingi na hatosalimika anaekeuka misingi hayo na adhabu iumizayo, na atakae fuata misingi hayo atapata utukufu na heshima hapa duniani na kesho akhera, na miongoni mwa misingi hayo ni swala, swala ambao ni msingi wa dini na nguzo ya pili baada ya kutamka shahada mbili, na swala ni fadhila kubwa ambapo Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) amesema: [ Swala ni bora, na atakae weza kuzidisha basi na azidishe].

Swala ni nguzo ya pili katika uislamu. Imepokewa na Anas akisema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) : [Nimependekezwa na wanawake mafuta mazuri na nikajaaliwa kuwa swala ndio kitulizo cha macho yangu]. Na ni ibada ya kwanza aliyofaradhisha Mwenyezi Mungu, na mwanzo atakayohisabiwa mwanadamu, na ndio wasia wa mwisho ambao Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) ameusia umma wake akisema: [ Swala, swala na watumwa wenu]. Na ndio mwanzo itakayopotea na ikipotea imepotea dini.

Na kuonyesha umuhimu wa swala kufaradhishwa katika mbingu ya saba, na ndio inaowekwa mafungamano kati ya mja na mola wake, na inakataza maovu. Amesema Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala):

قال تعالى) : إِنَّ الصَّلَاةَ تَنْهَى عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنْكَرِ( [العنكبوت: 45] {{Hakika Swala humzuilia huyo mwenye kusali na mambo machafu na maovu}}

Wengi miongoni mwa watu wanaswali swala ya ghurabu (kudonoa), hawana utulivu, wala hawamtaji Mwenyezi Mungu ila kwa uchache, kugeuka katika swala kujikuna, mfanya biashara kufikiria mali yake anaposwali.

Hadithi iliopokewa kutoka kwa Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) akimuambia mtu ambae hakua na utulivu katika swala “Rejea ukaswali kwani hujaswali”

Mambo Ambayo Husababisha kuhudhurisha Moyo unapokuwa katika Swala

Mambo ambayo husababisha kuhudhurisha moyo ni kujua unacho kizungumza au unachokifanya, mfano;

Unapotoa Takbir na kuinua mikono miwili hii inamaanisha kumtukuza Mwenyezi Mungu.

Na ukiweka mkono wa kulia juu ya kushoto ni kujidhalilisha mbele ya Mwenyezi Mungu.

Na ukirukuu inamaanisha kumuadhimisha Mwenyezi Mungu.

Na ukisujudu ni kunyenyekea kwa Mwenyezi Mungu.

Anaposema: “Shukrani zote ni za Mwenyezi Mungu” anaitikia Mwenyezi Mungu amenishukuru mja wangu, na anaposema “ Mwenye kuneemesha neema kubwa kubwa na neema ndogo ndogo” anasema Mwenyezi Mungu: amenisifu mja wangu, na anaposema mwenye kumiliki siku ya mwisho, anasema Mwenyezi Mungu: amenitukuza mja wangu., anaposema kwako wewe nakuabudu na kwako wewe nataka msaada, anasema Mwenyezi Mungu: haya ni kati yangu na mja wangu.

Anaposema ametakasika Mola wangu aliekua mkubwa, na ukisema ametakasika mola wangu alie juu, Mwenyezi Mungu anasikia hata kama ni kwa sauti ya chini, anasikia kila neno unalolisema na hata kama ni kwa sauti ya chini.

Kumuomba Mwenyezi Mungu usaidizi wa kufanya amali nzuri, imepokewa na Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) akisema: [Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie katika kukutaja na kukushukuru, na kufafanya uzuri ibada yako].

Kujua kuwa unyenyekevu ni roho ya swala, Amesema Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala):

قال تعالى (الَّذِينَ هُمْ فِي صَلَاتِهِمْ خَاشِعُونَ ) [المؤمنون: 2]

{{Ambao katika Sala zao huwa ni wanyenyekevu}}.

Wito wa kuhifadhi Swala

Amesema Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala):

قال تعالى) : حَافِظُوا عَلَى الصَّلَوَاتِ وَالصَّلَاةِ الْوُسْطَى). [البقرة: 238]

{{Angalieni sana Sala – zote kuzisali kwa jamaa- Na khasa ile Sala ya kati na kati}}.

Amesema Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala):

قال تعالى : قَدْ أَفْلَحَ الْمُؤْمِنُونَ1 الَّذِينَ هُمْ فِي صَلَاتِهِمْ خَاشِعُونَ [المؤمنون1: 2]

{{Kwa hakika wamefaulu waumini. Ambao katika Sala zao huwa ni wanyenyekevu}}.

Na akasema tena Mwenyezi Mungu(Subhaanahu wa Taala):

قال تعالى) : وَالَّذِينَ هُمْ عَلَى صَلَوَاتِهِمْ يُحَافِظُونَ 9أُولَئِكَ هُمُ الْوَارِثُونَ 10الَّذِينَ يَرِثُونَ الْفِرْدَوْسَ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ )[المؤمنون9: 11]

{{Na ambao Sala zao wanahifadhi. Hao ndio warithi. Ambao watarithi pepo; wakae humo milele}}.

Khutba ya pili

Ndugu Waislamu, Hakika Sala ni nguzo muhimu katika dini ya kiislamu. Bali Uislamu wa mtu haukamiliki bila ya Sala. Na Nguzo hii ndio ya kutafautisha baina ya Muislamu na kafiri. Amepokea Jabir hadithi kutoka kwa Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) akisema: “Kati ya Muislamu na kafiri ni kuwacha swala” na akasema tena Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam): [ Tofauti kati yetu na wao ni kuacha swala, atakae wacha swala ni amekufuru]. amepokea ‘Abdillah bin Shakik Ukeili, amesema maswahaba yake Mtume walikuwa hawaoni ukafiri isipokua ni kuacha swala.

Umuhimu wa kuswali Swala ya Jamaa.

Ndugu katika imani, Sala ya jamaa ni wajibu kwa wanaume. Hadithi za Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) zimeweka wazi jambo hili. Amepokea Ibn Abbas hadithi kutoka kwa Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) akisema: [ Mwenye kusikia adhana na asijibu basi hana swala isipokua mwenye udhuru]. Amepokea Abu-Hureira amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) : [ nimeazimia kuamrisha pote la watu waniletee kuni, kasha niwaendee waja wasiokuja kuswali swala kwa jamaa nichome nyuma zao].

Kuwahimiza Watoto kuswali na kuwalea kwa Mfumo huo

Watoto ni neema ya Allah (Subhaanahu wa Taala) kwa waja wake. Na neema ikiwa ni ya Allah ni lazima ichungwe kulingana na matakwa yake Allah. Mwenyezi Mungu Alipotupatia neema hii, Hakutuacha tuitumie neema hii kama tunavyotaka sisi, bali Yeye Mwenyewe Alichukua jukumu la kutufundisha namna ya kuitunza neema hii kupitia kwa mafundisho ya Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam). Na miongoni mwa mafundisho hayo, ni kuwafundisha watoto Sala wakiwa wadogo kuanzia miaka saba. Amesema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam): [Waamrisheni watoto wenu kuswali wakiwa na miaka saba, na wapigeni wakiwa na miaka kumi].

Na Mwenyezi Mungu Akututahadharisha tusiwe ni wenye kupuuza jukumu hilo.

Amesema Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala):

(يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آَمَنُوا قُوا أَنْفُسَكُمْ وَأَهْلِيكُمْ نَارًا ([التحريم: 6]

{{Enyi mlioamini, Jiokoeni nafsi zenu, na watu wenu, na moto ambao kuni zake ni watu na mawe}}. Na ameseme Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala):

وقال تعالى) : وَأْمُرْ أَهْلَكَ بِالصَّلَاةِ وَاصْطَبِرْ عَلَيْهَا ([طه: 132]

{{Na waamrishe watu wako kusali, na uendelee mwenyewe kwa hayo}}.

Mwisho

Ndugu katika imani, Sala ni jambo kubwa lina uzito mkubwa katika Dini yetu. Muislamu akiacha kusali basi ajuwe yuko katika hali mbaya, ikiwa ataendelea na hali hiyo mpaka afikiwe na mauti basi mwisho wake ni mabaya. Kwa hivyo, tufanyeni bidii kuhifadhi Sala kwa wakati wake. Na miongoni mwa kuhifadhi sala ni kuisoma na kuifahamu kama alivyofundisha Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam), ili uweze kuitekeleza kama alivyo kuwa akitekeleza Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam). Tunamuomba Allah Atupe tawfiq ya kuweza kutekeleza sala kwa wakati wake. Na tuweze kusali kama alivyo kuwa akisali Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam).





Vitambulisho: